Posts

Showing posts from December, 2018

Hizi ndio faida za kumkumbatia mumeo/mkeo

Image
Umewahi kufikiria faida zinazopatikana kwa kumkumbatia mkeo mkiwa mmelala? Famasia yako ya Ndoa Maridhawa inakuletea faida 6 za kukumbatiana kitandani: 1. HUPUNGUZA SHINIKIZO LA KISAIKOLOJIA: Unapomkumbatia mkeo mkiwa mmelala husaidia kuzalisha kichocheo (homoni) cha furaha kiitwacho oxytocin. Homoni hii hufanya kazi ya kupunguza hatari ya kupatwa na maradhi ya moyo na kupunguza shinikizo la kisaikolojia. Hilo pia hupelekea kupunguza hatari ya kupatwa na maumivu ya kichwa na maradhi mengine. 2. USINGIZI MARIDHAWA: Wanandoa wanapokumbatiana husaidia kulala vizuri. Tafiti mpya zimeonesha kuwa kumbatio hupunguza cortisol na hivyo kupunguza shinikizo la kisaikolojia. Pindi cortisol inapopungua mwilini, moja kwa moja usingizi huwa mzuri na mwanana. 3. Unapomkumbatia inaweza kusababisha raha, hasa mambo yanapofikia kwenye hatua ya kucheza, lakini kabla ya hapo furahia ladha ya mgusano wa ngozi zenu kabla ya kusonga mbele… Moyo wako unatakiwa kuuhudhurisha katika eneo na muda wa mgusano hu...

Tabia hatari kwa mwanamke katika mapenzi

Image
Kiasili na kitamaduni, mwanaume hupenda kutawala ama kuhisi anatawala. Mwanaume akiona ama akihisi anatawaliwa na mwanamke, hata akiacha kusema hujikuta akianza kujihisi vibaya kuhusu nafsi yake na hatimaye kuhusu huyu mwanamke anayehisi anamtawala. Katika uhusiano wanawake wengi hukosea kwa kuamini, ukali ama kuwa na maneno mengi ya kuudhi ni njia nzuri ya kupambana na wanaume zao katika yale mambo wanayowahisi. Kitu wanachosahau kukiwaza ni kwamba wanaume huchukia kufokewa, kufanywa wajinga na kuhisi wanatawaliwa na wanawake. Na mwanamke mwenye tabia hizo za kufoka kwa mume ama mpenzi wake, tabia ya kujihisi anamtawala mume wake sio tu anamtesa mume wake kifikra ila pia anatengeneza mazingira ama ya huyu mwanaume kuachana naye, kuwa na mwanamke wa pembeni ama kupenda kukaa mbali na mwanamke huyu. Wanaume wengi wakiwa kazini wanajikuta wako huru na amani zaidi kuliko wakiwa na wake zao. Pia wako wanaume wengi msisimko wa kihisia na wapenzi wao umeisha ama umepungua kwa asilimia ku...

Anachohitaji mwanamke kutoka kwa mwanaume wake

Image
Katika mahusiano mwanamke anakua anahitaji mambo mbalimbali lakini si yote atakua anamwambia mpenzi wake au mume wake. Kichwani mwake anajua kama unampenda basi vitu hivyo hautavisahau. Sasa hapa ndugu zangu wanaume inapasa kuchekecha akili na kujiongeza kwa maana vitu hivi huwa vinasaidia kuendelea kuwaweka karibu katika mahusiano. Leo tutaangalia baadhi ya vitu ambavyo mwanamke/mke anavihitaji kutoka kwa mwanaume/mme wake.. 1. Kutomuonesha mfumo Dume, sio lazima kwenye kila jambo basi uwe unaweka na kutanguliza mfumo dume. Siku nyingine jishushe kwa mkeo/mwanamke wako itasaidia kumvuta karibu na kuongeza mapenzi kwako. 2. Mpe sikio, hakikisha unamsikiliza mke wako anapokua anakueleza jambo. Na hapa unatakiwa umsikilize kwa makini akiwa anakueleza mambo ya msingi na mambo ya utani pia. Muda mwingine mwanamke anahitaji kusikilizwa tu roho yake inatulia. 3. Zawadi, mwanamke anapenda kupewa zawadi hivyo ni vema ukawa na utaratibu wa kumpa zawadi mke wako hata kama ni vitu vidogo vidog...

Njia bora ya kuishi na Mwanaume/Mwanamke mwenye hasira

Image
Nani hajawahi kupata hasira kwa mwenza wake? hakuna mtu, Si ndio? ni katika sehemu yoyote ya mahusiano, lakini tumekuwa tukiamini kwamba Hasira ni mbaya, na kwa sababu hio hatutakiwi kuwa na hasira Kwa hio hatujui jinsi ya kuishi na mke au mume mwenye Hasira. ni kweli , ni moja ya njia nzuri ukiwa ni mwenye hasira kwa mwenza wako. kitu gani zaidi kinatokea? Hasira yako inaweza kuwa ni kitu kizuri kwenye mahusiano yako. inaweza kuonekana kama kuchanganya hivi, lakini kuwa mke au mume mwenye hasira inaweza kuwa isiwe kitu kibaya. Kwa nini, ngoja tuendelee kusoma hapa. Hasira Ni Kawaida. Hasira huja kutokana na kitendo kilichotokea wakati huo, lakini mara nyingi sana, Tunakosa nafasi ya kuelezea hisia zetu za hasira  zinapokuja. Na yote hio hutokea kwa sababu ya kuogopa au kuona aibu kuwa na hasira.kwa hio , kwa akili tulizonazo,Tunaficha hasira. Na tusiposhughulikia hilo , hasira inatushughulikia! Kwa mfano ,Hasira ndogo inaweza kugeuka ikawa hasira kubwa- kitu ambacho ni hatari n...

Dalili nne ambazo ukiziona kwenye mahusiano ujue mnaendana

Image
Wataalamu wa mahusiano wanasema kuwa kuna dalili nne ambazo ukiziona kwenye mahusiano yako basi amini kuwa ninyi mnaendana na pia mapenzi yenu yatadumu 1. Uhusiano wenu uwe na uwiano. Mahusiano ambayo yamefanikiwa ni yale yenye uwiano sahihi. Katika mahusiano mtakuwa tofauti wakati mwingine, na utofauti huu lazima ulete ulingano. Mfano, kuna ambao hupenda sana kutoka out na marafiki, huyu anahitaji kupata mtu ambaye si mpenzi sana wa kwenda out ili kuleta mlingano. Unatakiwa kuwa na mtu ambaye unakamilika unapokuwa nae, mtu ambaye mkiwa pamoja mkichanganya tabia zenu mnapata tabia moja ambayo imetokana na kuathiriana kwa matendo yenu. 2. Mnafurahia kusafiri pamoja. Njia rahisi kabisa ya kujua kama mnaendeana ni kama manafurahia mnapokuwa manasafiri pamoja, Watu wanaoendana hupenda kusafiri pamoja na kwenda sehemu tofauti tofauti.  Kama wewe unataka kusafiri kwa gari, lakini mwenzako anataka kupanda ndege na ubishani wenu unakuwa mkubwa basi ujue ninyi manatatizo. Wapenzi wanaoen...

Kanuni za kuchagua mpenzi sahihi katika mahusiano

Image
Mwalimu wetu wa hesabau alikuwa akitumbia ili upate hesabu unatakiwa kujua kanuni za kufanya hesabau hizo, na kama ilivyo katika kufanya maswali ya hesabu basi hata katika mahusiano ipo hivyohivyo pia  ili upate mwenza aliyebora kwako unatakiwa kujua kanuni za kumpata mwenza sahihi kwako kama ifutavyo: Chagua mtu mwenye msimamo Muda aliotumia mpenzi wako kudumu katika uhusiano wake uliopita unaweza kukupa ishara ya nguvu ya mtu kudumu na wewe; Unaweza kutumia njia hii kama kipimo cha matarajio ya uhusiano wenu mpya. Ikiwa, kwa mfano, mwenza wako anayetarajiwa alikuwa na mahusiano kadhaa ambayo yalidumu kwa muda mrefu takribani yenye utulivu wa miaka miwili au zaidi, hii inaelezea uwezo wake mzuri wa kujitoa. Kwa upande mwingine, mtu ambaye ana historia ya uhusiano usio thabiti, wa muda mfupi lazima aonekane kama hatari hata kama atatoa kile kinachoonekana kuwa ni sababu za halali. Kamwe haiwezi kuwa kosa la mtu mwingine kila mara anapovunja uhusiano. Chagua mtu mwenye mfano mzur...